MAMA VANESSA SEHEMU YA NANE

Katika kitu ambacho Lucas huwa kinamnyima raha ni kuona mwanamke akilia mbele yake. Yaani yeye mwanamke akijilIza basi huwa anamwamini kupita kiasi. Alimbembeleza mpaka Mama Vanesa akanyamaza. Kwikwi zilimkaba sana na alikuwa akiona kabisa kijana huyo ameonewa. Mwanzo hakuwa na ushahidi wa moja kwa moja lakini zile picha zinazomuonesha mme wake akiwa na mke wa Lucas zilimuuma kupita maelezo.
“Kwa hiyo haya yote yametokea nini sasa kifanyike” Lucas alihoji mara baada ya mama huyo kubembelezwa na kurudi katika hali yake ya kawaida.
“Ndo maana nimekuita hapa ili tupange mambo na ikibidi tumkomeshe”
“Wewe unataka tumfanyeje hili hali yeye ni boss mwenye fedha. Nikikuruka na kujifanya mjuaji sana ndo nafutwa kazi kabisa.”
“Siku zote usikubali kupoteza haki yako kisa kuogopa kufukuzwa kazi. Usikubali kunyang’anywa mke au hata uhuru wako kisa pesa. Nakuambia tukiungana mimi na wewe tutafanikiwa kwa hili. Dawa ya moto ni moto na hivi tunaushahidi, hiyo kazi huwezi kufukuzwa. Mimi ndo Emmy hilo jina la mama Vanessa ni la heshima tu.
“Sawa Emmy ingawa nitapenda kukuendelea kukita mama Vanesa ni jina zuri linatamika vizuri. Ingawa mtu anavuta taswira laba ni mama kweli”.
“Kila mwanamke ni mama maana hata kama bado hajazaa ipo siku atakuja kuzaaa”. Sio mbaya ukiiita hivyo maana hata Vanesa mwenyeewe anajua kuwa mimi ndo mama yake. Alifafanua mama huyo.
“Sawa lakini bado sijajua mpango mkakati ni upi?
“Ni mdogo tu ukitendwa tenda, ukipendwa pendwa”.
Maneno hayo yalikuwa bado yanamuacha njiapanda Lucas Manyama hakujua mwanamke huyo alikuwa akitaka nini hasa kutoka kwake. Maneno hayo kwake yalikuwa yakiahshiria kuwa mama huyo alikuwa akitaka alipe kisasi kwa wao kuwa wapenzi. Kuna vitu vilikuwa vikimtatiza kwanza kwa nini mama huyo alichagua njia hiyo ya kulipa kisasi kwa nini wasipeleke ushahidi a idara ya kazi na kueleza kuwa alikuwa akisimamishwa kazi kwa sababu ya hujuma za boss wake ambaye alitumia uboss kuwa na uhusiano wa kimapenzi na mkewe. Hili jambo lilimuumiza sana hasa akikumbuka ni mbali sana alipotoka. Alifikiria jinsi alivyomsomesha mke wake tena kwa tabu mpaka akafanikiwa kupata elimu na baadaye kazi. Alifikiria tukio la yeye kusimamishwa kazi na kuona kabisa haikuwa sawa. Wakati Lucas akiwaza na kuwazua mara simu ya mama Vanesaa ikaita.
Mama Vanesaa aliangalia na kusita kupokea maaana aliyekuwa akipiga ni baba Vanessa. Simu haikukukoma maana ilivyokata ikapigwa tena na safari hii mama Vanesaa alipokea.
“Upo wapi mke wangu maana ndo nimerudi kutoka Mwanza kwenye semina nimefika nyumbani sijakukuta?”
“Nimetoka kidogo mme wangu na si muda mrefu nitakuwa hapo kuna vitu tu nilienda kuvinunua kwa ajili ya safari yangu ya kesho.”
“Sawa huwai kurudi basi maana nimekumisss sana na nimekuletea zawadi nzuri mke wangu..
“Usijali honey nakuja”.
Lucas Manyama alikuwa ametega sikio na kusikiliza kila kitu kilichokua kikzungumzwa. Aliisikia vyema sauti ya boss wake. Roho ilimuuma na hakutarajia kwa picha zile zikimuonesha mke wake na boss wake wamekumbtaina wakicheza musiki Mama Vanesa angeweza toa majbu ya kukera yenye hasira. Na mama Vanesa hasingeongea hivyo kama vile hakuna kitu kibaya kilichotokea. Alitarajia mwanamke huyo atamtukana mwenyewe.
“Samahani boss wako amepiga na usiumie kwa mimi kuongea naye vizuri. Cha msingi tambua namtafutia dawa ya kumkomesha na mimi siku zote maishani mwanangu huwa sipendi kukurupuka na iktokea tatizo huwa natafuta njia ambayo itamuumiza muhusika. Kwa hiyo mkakati upo hivi mimi naenda Dar nitakaa kwa muda wa wiki moja kisha nitardi. Baada ya hapo tutakutana lakini nakuomba kwa wakati huu tuwe makini sana usikurupuke katika maumivu tufanya kama hakuna kibaya cha kuumiza moyo kilichotokea. Mama Vanesaa baada ya kusema hayo alifungua pochi yake na kutoa burungutu la pesa na kumkabidhi. Alitabasamu na kumuaga. Lucas alitamani amwambie hasiondoke lakini tayari ilikuwa ni hatari kama mme wake alishakuwa mjini. Mme wake licha ya kuwa boss katika benk ambayo alikuwa akifanya Lucas pia alikuwa ni mfanyabiashara hapo Musoma na nadiriki kusema alikuwa tajiri. Mama Vanesaa kazi yake kubwa ilikuwa kusimamania biashara hizo. Kwa hiyo ni mwanamke ambaye alikuwa akikutana na pesa karibu kila siku.
Kwa Lucas kupewa fedha ilikuwa zaidi ya ushindi kwa sababu alikuwa hana pesa kabisa. Yaani mfukoni alikuwa amebakiza shilingi elfu 10 na tayari account yake ya benk ilikuwa ikisoma ziro.Baada ya mama Vanesa kuondoka yeye alihesabu zile pesa na kukuta zilikuw laki moja. Alitabasamu na kusema asante Mungu kwa kuendelea kumsaidia kupitia watu.Aliamua kuondoka eno hilo maana anajijua kabisa akikaa baaa hachelewi kuanza kutamani kunywa pombe. Alimwita muhudu akamlipa na huyo akaeleka zake nyumbani kwake alipopangisha mitaa ya Iringo. Alifika akawasha Tv na kuendelea kuangali movie. Lengo lilikuwa ni kupoteza muda na mawazo aliyokuwa nayo. Alimwanza mama Vanesa jinsi alivyoumbika akashindwa kuelewa kwa nini boss wake hatulii wakati ana mke mzuri.
Siku ikawa imeisha hivyo na usiku mama Vanesaa alimtumia sms akimtakia usiku mwema. Usiku pia alimkumbuka Juliaana binti ambaye alimpa mapenzi usiku wa jana na kumfanya hasahu shida kwa muda. Alifikiria mengi na kujikuta akinyanyua simu na kumpigia rafiki yake Kimaro. Alikumbuka fadhila ambazo alimtendea na alimweleza kilichoendelea baada ya yeye kufika Musoma.
“Hapo mbaba ndo muda wa kulipa kisasi boss si kakupokonya mke wako na wewe fanya kweli. Tena kwa jinsi ulivyonielezea ni kwamba huyo mwanamke anataka duduuu.
Kimaro alabaki akiangua tu kicheko na kumwambia yeye anachohofia ni kushindana na watu wenye pesa maana kazi atakosa na gerzani ataingia.
“Kuhusu kazi usiogope mbaba nitakutafutia hata sehemu ya kujishikiza ila wewe kula huyo sijui mama Vanessa. Na ukifanikiwa nipigie picha mkiwa naye chumbani mimi nitajua cha kufanya. Nitalipa ghali ….aaaaaaaaaaaaaah. Hapa ni mjini hatuwezi sumbuliwa na mtu sijui kisa ana vichenji.”
Wakati wakiendelea kuongea na kupeana mbinu mbaya za kupambana na matatizo yaliyotokea simu ya Lucas ilikuwa ikiita. Alivyokata tu ikaita tena na kuangalia alikuwa Mishel mke wake wa ndoa.
*************ITAENDELEA

Comments

Post a Comment

Popular posts from this blog

Jinsi Ya Kumtambua Mwanamke Mwenye Nyege

JINSI YA KUCHEZEA MATAKO YA MWANAMKE NA KUMPA RAHA YA AJABU KWA KUYABINYA KATIKA MIELEKEO MAALAM SOMA HAPA

Kanga Moja....Ndembe Ndembe. Sehemu ya Kwanza